Write your own article idiot!
error: Content is protected !!

Monday, June 25, 2018

KISWAHILI: FORM FOUR: Topic 6 - UFAHAMU

 Join Our Groups

TELEGRAM | WHATSAPP


Schemes of Work 2024


English Course - Free


Kenya Resources








TOPIC 6: UFAHAMU

UFAHAMU WA KUSIKILIZA

Ufahamu wa kusikiliza ni zaidi ya kusikiliza tu kile kilichosemwa; badala yake ni uwezo wa mtu kuelewa maana ya maneno anayoyasikia na kuweza kuhusiana nayo kwa namna fulani. Kwa mfano mwanafunzi anaposikiliza hadithi, ufahamu mzuri wa kusikiliza humsaidia kuielewa hadithi hiyo, kuikumbuka, kuijadili, na hata kuisimulia tena kwa maneno yake mwenyewe.


Kujibu Maswali ya Habari Uliyosikiliza

Ufahamu wa kusikiliza unahusisha michakato kadhaa katika kuelewa na kupata maana ya kile kinachozungumzwa. Michakato hii inahusisha:
  • Kuelewa vizuri sarufi ya lugha ile inayozungumzwa
  • Kuelewa vyema maana ya maneno ya mhusiaka anayezungumza
  • Kuelewa sintaksia (muundo wa maneno) ya sentensi kwa namna zinavyowasilishwa.


Katika ufahamu wa kusikiliza, msikilizaji hana budi kuzingatia mambo yafutayo:

1. Kuwa makini na kuelekeza akili yote kwa mzungumzaji ili kuweza kusikia kila anachokisema.

2. Kutilia maanani vidokezo vya maana ili kubaini iwapo msemaji anaongeza jambo jipya, anatofautisha, anafafanua au anahitimisha hoja.

3. Msomaji anatakiwa kuandika baadhi ya mambo anayoona kuwa ni ya muhimu ili kumasidia kukumbuka hapo baadae.

4. Kuwa makini na ishara mbambali za mwili kama vile kurusha mikono, kutingisha kichwa, kutingisha mabega au hata kupepesa macho. Ishara hizi huwa zinachangia kwa kiasi kikubwa kupata maana katika mazungumzo.


Kufupisha Habari

Ili kuandika ufupisho mzuri wa habari uliyoisikiliza yafuatayo hayana budi kuzingatiwa; kusikiliza habari kwa makini ili kuielewa vizuri, kuandika mawazo makuu yanayojitokeza katika kila aya, kuyaunganisha mawazo makuu na kuiandika habari kwa maneno yako, kuhesabu idadi ya maneno kama inazidi na kuandika idadi hiyo mwisho wa ufupisho upande wa kulia chini kidogo.

Ufahamu wa Kusikiliza
Zoezi
Soma habari kisha toa ufupisho wake


UFAHAMU WA KUSOMA

Ufahamu wa kusoma ni ule mtu anaoupata kwa njia ya kusoma makala, kifungu cha habari, kitabu au gazeti.

Kujibu Maswali kutokana na Habari ndefu uliyosoma
Kuna vipengele viwili vinavyounda mchakato wa ufahamu wa kusoma:
  • Uelewa wa msamiati na
  • Uelewa wa matini
Ili kuilelewa habari/matini ni lazima msomaji awe na uwezo wa kuelewa msamiati uliotumika katika matini hiyo. Endapo maneno yaliyotumika hayataeleweka vilevile matini yote hataeleweka.


Katika ufahamu wa kusoma, msomaji anatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo:

1. Kubaini mawazo makuu; msomaji anaposoma habari fulani au kitabu inatakiwa ajiulize, Je, kinachoongelewa hapa ni nini? Ni jambo gani hasa analolizungumzia mwandishi? Msomaji akiwa na maswali haya akilini mwake basi itakuwa rahisi kwake kuielewa habari hiyo.

2. Kuzingatia alama za uakifishi; msomaji ni lazima azingatie alama za uakifishi, kwa kufanya hivyo itamsaidia kuelewa ujumbe wa habari hiyo na endapo hatazingatia alama za uakifishaji anaweza kupotosha maana ya mwandishi.

3. Kubaini maana ya maneno na misemo mbalimbali; habari nyingine huwa zina maneno ya kisanaa hivyo ni muhimu msomaji kubaini maana ya maneno hayo katika muktadha wa habari hiyo, hii itamsaidia kuelewa vyema maana ya mwandishi.

4. Vilevile msomaji anatakiwa kumakinikia kile anachokisoma, kila kipengele anachokisoma inampasa akielewe vizuri.

Kwa kuzingatia haya yote msomaji atakuwa na uelewa mzuri juu ya habari aliyoisoma na pia anaweza kufupisha habari hiyo aliyoisoma.


Kufupisha Habari

Kufupisha habari ni kuandika upya habari uliyoisoma kwa maneno machache lakini bila kupotosha ujumbe wa habari ya kwanza.

Ufupisho wa habari huwa na sifa hizi:
  1. Huwa ni mfupi kuliko habari ya mwanzo
  2. Huwa na ujumbe uleule uliokuwa katika habari ya mwanzo
  3. Hujumuisha mawazo makuu yaliyodondolewa kutoka kwenye habari ya mwanzo
  4. Mawazo haya sharti yapangwe katika mtririko wenye mantiki
Ufahamu wa Kusoma


Hatua za Kufuata katika Kuandika Ufupisho

Ili kuweza kufanikiwa kufupisha habari kwa ufanisi hatua zifuatzo sharti zifuatwe:

1. Kuisoma au kuisilikiza habari kwa makini ili kuielewa vizuri

2. Kutambua na kubaini mawazo makuu yanayojitokeza katika kila aya

3. Kuyaunganisha mawazo makuu na kuandika au kuelezea ufupisho wa habari hiyo kwa maneno yako mwenyewe bila kupostosha maana ya habari ya kwanza.

4. Kuhesabu idadi ya maneno ya ufupisho ili kuyapunguza ikiwa yanazidi idadi iliyotakiwa.

5. Kama muda unaruhusu pitia tena habari ya mwanzo na pitia tena ufupisho ili kujiridhisha kuwa hujaacha taarifa yoyote ya muhimu.


Kufupisha Habari ndefu uliyosoma

Ili kuweza kuandika ufupisho wa habari ndefu uliyoisoma hatua zifuatazo sharti zifuatwe, kusoma habari kwa makini na kuielewa vizuri, kubaini mawazo makuu, kuandika ufupisho wa habari kwa maneno yako, kuhesabu idadi ya maneno na kupunguza yaliyozidi na kupitia tena habari ya mwanzo na ya mwisho kama muda unaruhusu. Aidha ufupisho wa habari huwa ni mfupi na una ujumbe uleule wa habari ya mwanzo.










EmoticonEmoticon